Jumatatu 20 Oktoba 2025 - 07:47
Maandamano dhidi ya Trump yafanyika maeneo yote ya Marekani

Hawza/ Maandamano makubwa yakiwa na kaulimbiu isemayo “Hapana kwa Ufalme!” yamefanyika katika miji mikubwa kadhaa ya Marekani, ambapo wananchi wameonyesha hasira na upinzani wao dhidi ya sera potovu za Trump kuhusu wahamiaji, elimu, na nyanja nyinginezo. Waandalizi wa maandamano haya wanaamini kuwa mikusanyiko hii imefanyika katika matukio takribani 2,600 kote nchini Marekani.

Kwa mujibu wa Kitengo cha tarjama cha Shirika la Habari la Hawza, maandamano haya makubwa ni mkusanyiko wa tatu wa wananchi tangu kurejea kwa Trump Ikulu ya White House. Miongoni mwa sababu zilizopelekea kufanyika kwa maandamano haya ni kufungwa shughuli za serikali kuu, jambo lililosababisha kusitishwa kwa huduma na programu za serikali ya shirikisho. Wataalamu wanaona hali hii kuwa ni jaribio la Trump kupima mizani ya nguvu za nyuklia na mamlaka binafsi katika mchezo huu wa kisiasa, huku ikionekana wazi kuwa sasa taasisi ya utendaji (serikali kuu) nchini Marekani imeanza kuonesha mienendo ya kichokozi dhidi ya Bunge na Mahakama. Hali hii, kwa mujibu wa wachambuzi, ni hatua hatari inayorudisha taifa hilo katika mfumo wa kiimla na udikteta wa utawala.

Waandaaji wa tukio hili kubwa wamesisitiza kuwa mikusanyiko hiyo imefanyika katika zaidi ya matukio 2,600 nchini Marekani.

Inapaswa kusemwa pia kuwa maandamano haya yalianza nje ya Marekani, yakianzia mbele ya Ubalozi wa Marekani mjini London, ambapo mamia ya waandamanaji walikusanyika, kisha wakiungwa mkono na mamia wengine katika miji ya Madrid na Barcelona. Baadaye, kaulimbiu hii ya “Hapana Ufalme!” ikawa wimbo mkuu wa maandamano ya wananchi kote Marekani.

Chanzo: Al Jazeera

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha